Wizara ya Maji

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)

TIRA Logo
TAARIFA KWA UMMA - KUANZA USOMAJI MITA ZA MAJI DAR ES SALAAM NA PWANI
10 Oct, 2025 Pakua
TAARIFA KWA UMMA - KUANZA USOMAJI MITA ZA MAJI DAR ES SALAAM NA PWANI

TAARIFA KWA UMMA

KUANZA USOMAJI MITA ZA MAJI DAR  ES SALAAM NA PWANI

10.10.2025

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) inawaatarifu Wateja na Wananchi katika Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani, kuwa zoezi la usomaji mita za maji litaanza Oktoba 10 hadi 15, 2025.

Baada ya zoezi la usomaji mita  kukamilika, Mteja atapokea ujumbe wa kuhakiki usomaji wa mita yake kabla ya bili kutumwa.

Kwa taarifa zaidi wasiliana nasi kupitia Kituo cha huduma kwa wateja 181 (Bure) na 0735 202121 (WhatsApp tu)

Imetolewa na 
Kitengo cha Mawasiliano