Wizara ya Maji

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)

TIRA Logo
TAARIFA KWA UMMA - KUZIMWA KWA MTAMBO WA RUVU JUU KURUHUSU MATENGENEZO MUHIMU
04 Sep, 2025 Pakua
TAARIFA KWA UMMA - KUZIMWA KWA MTAMBO WA RUVU JUU KURUHUSU MATENGENEZO MUHIMU

TAARIFA KWA UMMA

KUZIMWA KWA MTAMBO WA RUVU JUU KURUHUSU MATENGENEZO MUHIMU

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) inawatangazia Wateja na Wananchi  wanaohudumiwa kupitia Mtambo wa kuzalisha Maji Ruvu Juu uliopo Mlandizi Mkoani Pwani kuwa, kutakuwa na ukosefu wa huduma ya maji kwa muda wa saa 15, Septemba 4,2025  kuanzia Saa 12 asubuhi hadi Saa 3 usiku.

Sababu: Kuruhusu maboresho muhimu katika bomba kuu la kusafirisha Majighafi (Raw water) eneo la Mlandizi.

Maeneo yanayoathirika ni; 
Ruvu darajani, Ruvu JKT, Mlandizi, Mbwawa, Visiga, Mile 35, Misugusugu, Kongowe, Soga, Miembe Saba, Kwa Mfipa, Mwendapole, Tanita, Kwa Mathias, Kwa Mbonde, Picha ya Ndege, Lulanzi, Kibaha, Kiluvya, Kibamba, Mbezi, Magari Saba, Mbezi Inn, Mshikamano, Mbezi, Kimara, Kimara B, Kimara Korogwe, Bucha, Baruti, Ubungo, Makoka, Tabata, Kinyerezi, Kisukuru, Segerea, Msigani, Maramba Mawili, Vingunguti, Gongo la Mboto, Ukonga, Uwanja wa Ndege, Majumba sita, Kiwalani, Pugu na Kisarawe

Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kupitia kituo cha huduma kwa wateja 0800110064 (Bila Malipo) na 0735 202 121(WhatsApp tu)

Everlasting Lyaro
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano
DAWASA