Wizara ya Maji

Dar es Salaam Water Supply And Sanitation Authority (DAWASA)

TIRA Logo
TAARIFA KWA UMMA - TAARIFA YA KUKOSEKANA KWA HUDUMA YA MAJI KWA WAKAZI WA BAGAMOYO HADI ILALA
21 Aug, 2025 Pakua
TAARIFA KWA UMMA - TAARIFA YA KUKOSEKANA KWA HUDUMA YA MAJI KWA WAKAZI WA BAGAMOYO HADI ILALA

TAARIFA KWA UMMA 

TAARIFA YA KUKOSEKANA KWA HUDUMA YA MAJI KWA WAKAZI WA BAGAMOYO HADI ILALA
 

19.08.2025

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) inawajulisha Wananchi wanaohudumiwa kupitia Mtambo wa uzalishaji Maji Ruvu Chini kuwa, kutakuwa na maboresho yatakayoathiri upatikanaji huduma ya Maji kwa wastani wa Saa 12 

Muda: Siku ya Alhamisi, Agosti 21,2025 kuanzia Saa 1 Asubuhi hadi Saa 12 Jioni
Sababu: Kuruhusu maboresho ya kawaida ya Miundombinu katika Mtambo wa Ruvu Chini

Maeneo yatakayoathirika ni;
Bagamoyo, Mapinga, Mabwepande, Bunju, Tegeta, Mbweni, Boko, Kunduchi, Salasala, Goba, Madale, Mbopo, Mivumoni, Kawe, Lugalo, Makongo, Chuo-Kikuu Dar es Salaam (UDSM), Mwenge, Kijitonyama, Mikocheni, Msasani, Oysterbay, Masaki, hospitali ya Taifa Muhimbili, Mwananyamala, Kinondoni, Magomeni, Kigogo, Chang'ombe, Keko, Kurasini, Kiwalani, llala na katikati ya Jiji

Kukamilika kwa maboresho haya kutaimarisha kiwango cha uzalishaji na usambazaji Maji kwa Wananchi wanaohudumiwa na Mtambo huu.

Mamlaka inaomba radhi kwa usumbufu utakaojitokeza na inawasihi Wananchi kuhifadhi maji ya kutosha ili kukidhi mahitaji muhimu kipindi cha matengenezo.

Kituo cha huduma kwa wateja: 0800110064 (Bila malipo) na 0735 202121 (WhatsApp tu)


Everlasting Lyaro
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano
DAWASA