TAARIFA KWA UMMA - USOMAJI MITA ZA MAJI DAR NA PWANI KUANZA AGOSTI 10-15, 2024
							
							
							
							
							
						
					
                            
                                 10 Aug, 2024
                            
                                                        
                                 Pakua
                            
                                                    
                    TAARIFA KWA UMMA
USOMAJI MITA ZA MAJI DAR NA PWANI KUANZA AGOSTI 10 -15, 2024
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) inawataarifu wateja na wananchi katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani, kuwa zoezi la usomaji wa mita za maji utaanza Agosti 10 hadi 15, 2024.
Mamlaka inaomba ushirikiano kwa Wananchi pindi watoa huduma wa DAWASA watakapopita kutekeleza zoezi hili.
Baada ya zoezi la usomaji mita kukamilika, Mteja atapokea ujumbe wa kuhakiki usomaji wa mita yake kabla ya bili kutumwa.
Kwa taarifa zaidi wasiliana nasi kituo cha huduma kwa wateja 0800110064 (Bure) na 0735-202121 (WhatsApp tu)
Imetolewa na 
Kitengo cha Mawasiliano
            