Wizara ya Maji

Dar es Salaam Water Supply And Sanitation Authority (DAWASA)

TIRA Logo
TAARIFA KWA WAKAZI WA MBEZI JUU - MABORESHO YA DHARURA YATAKAYOATHIRI UPATIKANAJI HUDUMA YA MAJI
27 Jun, 2025 Pakua
TAARIFA KWA WAKAZI WA MBEZI JUU - MABORESHO YA DHARURA YATAKAYOATHIRI UPATIKANAJI HUDUMA YA MAJI

TAARIFA KWA WAKAZI WA MBEZI JUU

MABORESHO YA DHARURA YATAKAYOATHIRI UPATIKANAJI HUDUMA YA MAJI

26.6.2025

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) inawajulisha Wananchi wa Mbezi juu katika maeneo ya Jogoo, Baraza la Mitihani, St. Marry's na Vosel) kuwa kutakuwa na ukosefu wa huduma ya Maji kwa wastani wa Saa 24 kupisha matengenezo ya dharura.

Muda: Alhamisi, Juni 26, 2025 Saa 5 usiku hadi Ijumaa, Juni 27, 2025 kuanzia Saa 5 usiku.

Sababu: Kuruhusu maboresho dharula katika mfumo wa kusukuma Maji eneo la Mbezi juu Jogoo.

Maeneo yatakayoathirika ni;

Baraza la Mitihani, VOSEL Hotel, Mashine ya zamani, Bar mpya, Twiga street, Kanisa la Sabato, 34 street, Asante Grey, Mzee Lema, Msafiri street na Chongolo street.

Tunaomba radhi kwa usumbufu utakao jitokeza.

Kwa mawasiliano zaidi wasiliana nasi Kituo cha huduma kwa wateja 0800110064 (Bila Malipo) na 0735 202 121 (WhatsApp tu)

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano - DAWASA