Wizara ya Maji

Dar es Salaam Water Supply And Sanitation Authority (DAWASA)

TIRA Logo
TANGAZO LA DHARURA - KUZIMWA KWA MTAMBO WA UZALISHAJI MAJI RUVU JUU KWA SAA 24
11 Dec, 2024 Pakua
TANGAZO LA DHARURA - KUZIMWA KWA MTAMBO WA UZALISHAJI MAJI RUVU JUU KWA SAA 24

TANGAZO LA DHARURA

KUZIMWA KWA MTAMBO WA UZALISHAJI MAJI RUVU JUU KWA SAA 24


Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) inawatangazia Wateja na Wananchi wanaohudumiwa na mtambo wa kuzalisha maji Ruvu juu kuwa, kutakuwa na ukosefu wa huduma ya maji kwa muda wa saa 24 kuanzia siku ya Jumanne Desemba 10, 2024 kuanzia Saa 12 jioni hadi Saa 2 Asubuh ya Desemba 11, 2024

Sababu: Kuruhusu matengenezo ya bomba kubwa la inchi 40 linalopokea na kupeleka maji kwa Wananchi.
 
Maeneo yatakayoathirika ni; 
Chalinze, kijini cha Mboga, Ruvu Darajani, Ruvu JKT, Vigwaza, Mlandizi, Mbwawa, Visiga, Maili 35, Misugusugu, Kongowe, Soga, Miembe Saba, Kwa Mfipa, Mwendapole, Tanita, Kwa Mathias, Kwa Mbonde, Picha ya Ndege, Lulanzi, Kibaha, Kiluvya, Kibamba, Mbezi, Magari Saba, Mbezi Inn, Mbezi, Kimara,Tabata, Segere, Kinyerezi, Kisukuru, Bonyokwa, Msigani, Maramba Mawili, Kimara B, Kimara Korogwe, Bucha, Baruti, Ubungo, Magomeni, Ukonga, Uwanja wa Ndege, Kiwalani, Vingunguti, Gongo la Mboto, Pugu na Kisarawe

Wananchi wanashauriwa kuhifadhi maji kwa wingi na kuyatumia kwa matumizi muhimu zaidi.

Wasiliana nasi kupitia kituo cha huduma kwa wateja 0800110064 (bure) na 0735 202-121 (WhatsApp Tu)

Imetolewa na 
Kitengo cha  Mawasiliano