DAWASA CHALINZE NA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA
09 Oct, 2024

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) kupitia mkoa wa kihuduma DAWASA Chalinze, imeendelea kutembelea wateja katika Kata ya Bwilingu na Pera katika maadhimishio ya Wiki ya Huduma kwa wateja kwa lengo la kusikiliza changamoto na kuzipatia ufumbuzi ikiwemo kudhibiti uvujaji wa miundombinu, changamoto ya upatikanaji wa maji pamoja na kutoa elimu ya utunzaji wa miundombinu ya maji.
DAWASA imejipanga kuendelea kuwafikia wateja wengi zaidi ndani ya Wiki ya huduma kwa wateja iliyobeba ujumbe wa " Ni zaidi ya Matarajio".