Wizara ya Maji

Dar es Salaam Water Supply And Sanitation Authority (DAWASA)

TIRA Logo
HUDUMA YA MAJISAFI YAIMARIKA KIMARA
26 Oct, 2024
HUDUMA YA MAJISAFI YAIMARIKA KIMARA

 ● Ni baada ya matengenezo ya Mfumo wa umeme kukamilika

Wananchi mbalimbali wa mitaa ya Hawaii, Baruti  na Pentagon kata ya Kimara Wilaya ya Ubungo wameanza kupata huduma ya Majisafi kuimarisha  kufuatia kukamilika kwa matengenezo ya mfumo wa umeme katika mtambo wa uzalishaji maji Ruvu Juu yaliyokamilika hivi karibuni.

DAWASA imeshuhudia uimarikaji huo wa huduma wakati wa zoeI maalum la kupita katika mitaa mbalimbali ya kihuduma ili kubaini changamoto za Wakazi na kuzitatua.

Ndugu Sauda Abdallah, mkazi wa mtaa wa Hawaii amesema  kwa kipindi cha Matengenezo iliwalazimu Wakazi kununua maji kutoka 
maeneo ya mbali na wenginekutumia maji ya visima vya watu binafsi.

DAWASA inaendelea kufuatilia hali ya huduma ya maji katika maeneo mbalimbali yanayohudumiwa na mtambo wa Ruvu Juu ili kuondoa changamoto za kihuduma.