Wizara ya Maji

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)

TIRA Logo
"KUJITUMA KWENU KUTAJENGA DAWASA ILIYO BORA"- WAZIRI AWESO
04 Jul, 2024
"KUJITUMA KWENU KUTAJENGA DAWASA ILIYO BORA"- WAZIRI AWESO

Waziri wa Maji, Mhe.Jumaa Aweso (Mb) katika ziara yake leo Julai 4,2024 amekutana na Watumishi wa DAWASA - Kigamboni ambapo  amesisitiza kufanya kazi kwa bidii na kudumisha umoja ili kuleta maendeleo katika mkoa wa Dar es Salaam.

Mhe. Aweso pia ameelekeza uongozi wa DAWASA kuboresha huduma ya maji Kigamboni ili kila mwananchi anufaike na huduma ya Maji.