MABORESHO HUDUMA MIKENGE - KIMBIJI KAZI INAENDELEA
31 May, 2024

Kazi ya uboreshaji miundombinu katika kisima cha maji kilichopo eneo la Mikenge, kata ya Kimbiji iliyohusisha uchomeleaji wa pampu ya kusukuma maji ikiendelea kutekelezwa kwa kasi na mafundi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA).
Kukamilika kwa atengenezo hayo kutarejesha huduma ya maji kwa wakazi takribani 660 wa mitaa ya Kidagaa na Mikenge wilayani Kigamboni.