MABORESHO HUDUMA YA MAJI MWANDEGE- MKURANGA
30 Oct, 2024

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) Mkoa wa kihuduma Mkuranga imeendelea kuimarisha huduma kwa wateja kwa kufanya maboresho katika miundombinu ya maji katika chanzo cha uzalishaji maji cha Mwandege.
Kukamilika kwa kazi hii kutaimarisha upatikanaji wa uhakika wa huduma kwa wakazi takribani 491 wa maeneo ya Kilungule Juu, Kilungule Chini, Mwandege Magengeni, Kipara, Zahanati na Karoakoo
Ni kipaumbele cha Mamlaka kuhakikisha huduma zinatolewa kikamilifu nankatoka viwango bora kwa ajili ya ustawi wa jamii inayoihudumia.