MABORESHO YA HUDUMA YA MAJI MBOPO
14 Mar, 2025

Kazi ya matengenezo ya bomba la inchi 8 kwa lengo la kudhibiti uvujaji katika eneo la Mbopo wilaya ya Kinondoni ikitekelezwa na mafundi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) Mkoa wa kihuduma Mabwepande.
Kazi inahusisha kubadilisha sehemu ya bomba n kuweka lingine kwa umbali wa mita 150.
Kukamilika kwa kazi hii kutaboresha na kuimarisha huduma katika maeneo ya Mbopo, Loliondo, Mbopo centre na Zahanati.