Wizara ya Maji

Dar es Salaam Water Supply And Sanitation Authority (DAWASA)

TIRA Logo
USOMAJI NA UHAKIKI WA MITA UNAENDELEA TABATA
15 Jun, 2024
USOMAJI NA UHAKIKI WA MITA UNAENDELEA TABATA

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) kupitia Mkoa wa kihuduma Tabata unaendelea kuwakumbusha wateja juu ya umuhimu wa usomaji mita shirikikishi na uhakiki wa usomaji pindi wanapopata ujumbe mfupi baada ya zoezi la usomaji.

Afisa Biashara wa DAWASA Tabata, Ndugu Neema Mosha amesema  zoezi la usomaji wa mita kwa kushirikiana na wateja linaendelea sambamba na uhakiki wa usomaji ambapo wateja wanapata nafasi ya kuhakiki kabla ya kuandaliwa bili yake hii  husaidia kupunguza malalamiko pindi  bili zinapotumwa kwa wateja.

"Zoezi la usomaji mita bado linaendelea na baadhi ya wateja tayari wameshapokea jumbe fupi za uhakiki wa usomaji, tunatoa rai kwa wateja wetu  ni muhimu kuhakiki usomaji wako na kutoa taarifa kama kuna changamoto kupitia mawasiliano yetu rasmi au kufika katika ofisi zetu ili kutatua changamoto hizo kabla ya bili kutayarishwa" amesema Ndugu Mosha

Ndugu Mosha amesisitiza ushirikiano kati ya wateja na Mamlaka ni muhimu hivyo anaendelea kuwasihi wateja kutoa ushirikiano kwa watumishi pindi wanapopita katika makazi yao.

Mkoa wa kihuduma DAWASA Tabata una jumla ya wateja takribani 296,572 na unahudumia Kata za Tabat, Liwiti, Segerea, Kimanga, Kisukuru, Makuburi, Vingunguti, Kipawa, Mnyamani na Bonyokwa.