WANANCHI BANE WABORESHEWA HUDUMA
07 May, 2024

Maboresho ya miundombinu ya Maji yanayohusisha kubadilisha mabomba kwa wateja zaidi ya 200 mtaa wa Bane katika kata ya Pugu , wilaya ya Ilala inaendelea kutekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) kupitia Mkoa wa kihuduma Kisarawe.
Kazi inahusisha ubadilishaji wa mabomba ya muda mrefu ya inchi 2 yna kuweka mabomba mapya kwa umbali wa mita 750 ili kuwezesha upatikanaji endelevu wa huduma ya maji.
Kukamilika kwa kazi hiyo kutaimarisha upatikanaji wa huduma ya maji katika mitaa ya Bane kwa Mama flora, Bane kwa Kitabu na Bane Mabanda ya Kuku.