WAZIRI AWESO AFANYA KIKAO DAWASA
02 Dec, 2025
Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso (Mb) ameanza ziara Mkoani Dar es salaam kwa kufanya kikao na Bodi ya Wakurugenzi pamoja na Menejimenti ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) ili kuweka mikakati madhubuti ya uboreshaji huduma za Maji
Waziri Aweso anatarajia kukagua miradi ya maji na kuzungumza na wakazi wa Dar es Salaam katika Wilaya tatu za Mkoa wa Dar es salaam.
