Wizara ya Maji

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA)

TIRA Logo
UKOSEFU WA HUDUMA YA MAJI KIBAHA HADI KISARAWE
10 Feb, 2026 Pakua
UKOSEFU WA HUDUMA YA MAJI KIBAHA HADI KISARAWE

UKOSEFU WA HUDUMA YA MAJI KIBAHA HADI KISARAWE

 

10.2.2026

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) inawataarifu Wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani wanaohudumiwa na Mtambo wa Uzalishali Maji Ruvu Juu kuwa, kutakuwa na ukosefu wa huduma ya Majisafi kwa wastani wa Saa 9.

 

Siku: Jumatano 11 Februari, 2026.

Muda: Saa 3:00 Asubuhi hadi Saa 12:00 Jioni

Sababu: Kuruhusu matengenezo Kinga yatakayofanywa na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) katika Kituo cha kupooza umeme Mlandizi

 

Maeneo yatakayoathirika ni; 

Ruvu, Vigwaza, Mlandizi, Visiga, Misugusugu, Kongowe, Soga, Tanita, Kwa Mathias, Picha ya Ndege, Kibaha, Kiluvya, Kibamba, Mbezi, Kimara, Tabata, Segerea, Kinyerezi, Kisukuru, Bonyokwa, Msigani, Maramba Mawili, Kingazi, Ubungo, Magomeni, Ukonga, Uwanja wa Ndege, Kiwalani, Vingunguti, Gongo la Mboto, Pugu na Kisarawe

Mamlaka inaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

 

Wasiliana nasi kupitia 

Kituo cha Huduma kwa Wateja 181 (Bila malipo) na 0735 202121 (WhatsApp tu) 

 

Imetolewa na

Kitengo cha Mawasiliano