USIFUNGE PAMPU KWENYE MITA YA MAJI
							
							
							
							
							
						
					
                            
                                 04 Sep, 2025
                            
                                                        
                                 Pakua
                            
                                                    
                    
                    USIFUNGE PAMPU KWENYE MITA YA MAJI
Usifunge Pampu ya kuvuta Maji mbele au nyuma ya Mita yako. Kwakufanya hivyo utasababisha yafuatayo:
1. Kuvuruga msukumo wa upatikanaji wa maji kwa majirani zako.
2. Kusababisha majirani zako kukosa huduma ya Maji.
3. Kuharibu Mita/kupunguza ufanisi wa Mita.
ADHABU;
Sheria ya huduma za Majisafi na Usafi wa Mazingira No.5/2019 kifungu namba 61 kinazuia uharibifu wa miundombinu ya Maji. Ukipatikana na hatia adhabu yake ni faini kuanzia Tsh 500,000 hadi Tsh 50,000,000 na/au kifungo kuanzia Miaka miwili hadi Mitano.
            