MAANDALIZI KUZIMA MTAMBO WA MAJI RUVU CHINI SAA 14 YAMEKAMILIKA

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) imesema maandalizi muhimu kwa ajili kufanya matengenezo ya miundombinu ya bomba kuu la inchi 30 katika Mtambo wa uzalishaji maji Ruvu chini ulioyopo wilayani Bagamoyo, mkoani Pwani yamekamilika.
Meneja Mtambo wa uzalishaji Maji Ruvu Chini, Mhandisi Tyson Mkindi ameeleza kuwa ni matengenezo ya dharura kwenye bomba kuu la kupokea Maji.
"Timu ya ufundi imekamilisha maandalizi muhimu ya kuwezesha kazi ya matengenezo ambapo itakayopelekea kuzima mtambo wa Maji Ruvu Chini kwa wastani wa saa 14 i ili kufanikisha kazi hiyo" amebainisha Mhandisi Mkindi
Mhandisi Mkindi amesena kutokana na kuzimwa kwa kazi hiyo kutapelekea maeneo mbalimbali kukosa huduma ya maji ambayo ni: Bagamoyo, Mapinga, Mabwepande, Bunju, Tegeta, Mbweni, Boko, Kunduchi, Salasala, Goba, Mivumoni, Kawe, Lugalo, Makongo, Chuo - Kikuu Dar, Mwenge, Kijitonyama, Mikocheni, Msasani, Oysterbay, Masaaki, Upanga, Kariakok, Mwananyamala, Kinondoni, Magomeni, Kigogo, Chang'ombe, Keko, Kurasini, Kigamboni, Airport, Kiwalani, Buguruni, Vingunguti, Ilala na Katikati ya mji.