Wizara ya Maji

Dar es Salaam Water Supply And Sanitation Authority (DAWASA)

TIRA Logo
MABORESHO HUDUMA YA MAJISAFI KATA YA MLANDIZI-PWANI
20 Feb, 2025
MABORESHO HUDUMA YA MAJISAFI KATA YA MLANDIZI-PWANI

Kazi ya matengenezo ya bomba la inchi 6 yakiendelea kutekelezwa na mafundi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) katika eneo la Hai Village  kwa lengo la kuongeza msukumo  wa maji kwa wakazi wa mitaa  ya Mlandizi Kati na Mlandizi Mjini  katika Kata ya Mlandizi, Mkoani Pwani. 

Wateja zaidi ya 900 katika  maeneo ya Hai, Janga, Uwanja wa star, Kona pub, Msongola, Miti mirefu na Disunyara wanatarajiwa kupata huduma kwa msukumo mzuri baada ya kukamilika kwa kazi hii. 

DAWASA inaendelea na kazi ya kuboresha usambazaji wa huduma ya majisafi kwa wananchi kwa lengo la kuimarisha upatikanaji wa huduma kikamilifu.