Wizara ya Maji

Dar es Salaam Water Supply And Sanitation Authority (DAWASA)

TIRA Logo
MDAULA WABORESHEWA HUDUMA YA MAJI
20 May, 2024
MDAULA WABORESHEWA HUDUMA YA MAJI

Kazi ya uboreshaji wa miundombinu ya maji imetekelezwa na mafundi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) eneo la Msolwa kata ya Bwilingu Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze.

Kazi hiyo imehusisha matengenezo katika bomba la inchi 6 lililopata hitilafu.Kukamilika kwa matengenezo hayo kumerejesha huduma katika maeneo ya Msolwa, Mdaula, Chang'ombe na Matuli.