Wizara ya Maji

Dar es Salaam Water Supply And Sanitation Authority (DAWASA)

TIRA Logo
TAARIFA KWA UMMA - KUKOSEKANA KWA HUDUMA YA MAJI KWA WANANCHI WA MLANDIZI HADI KISARAWE
28 Sep, 2024 Pakua

TAARIFA KWA UMMA

 KUKOSEKANA KWA HUDUMA YA MAJI KWA WANANCHI WA MLANDIZI HADI KISARAWE

28.09.2024
 
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) inawatangazia Wateja na Wananchi  wanaohudumiwa na mtambo wa kuzalisha maji Ruvu Juu kuwa, kutakuwa na ukosefu wa huduma ya maji kwa wastani wa saa 7 siku ya Jumamosi Septemba 28, 2024 kuanzia Saa 5 Asubuhi hadi Saa 12 Jioni.

Sababu: Kupisha Matengenezo kinga katika kituo cha kupooza umeme Mlandizi kazi inayofanywa na Shirika la Umeme Nchini (TANESCO) 

Maeneo yatakayoathirika ni; 
Ruvu darajani, Ruvu JKT, Mlandizi, Mbwawa, Visiga, Mile 35, Misugusugu, Kongowe, Soga, Miembe saba, Kwa Mfipa, Mwendapole, Tanita, Kwa Mathias, Kwa Mbonde, Pichandege, Lulanzi, Kibaha, Kiluvya, Kibamba, Mbezi, Magari Saba, Mbezi inn, Mbezi, Kimara,Tabata, Kinyerezi, Kisukuru, Msigani, Maramba mawili, Tabata, Kimara B, Kimara Korogwe, Bucha, Baruti,Ubungo, Kisarawe, Ukonga, Pugu, Uwanja wa ndege, Majumba sita , Kiwalani na Gongo la Mboto na Kisarawe

Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.

Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kupitia kituo cha huduma kwa wateja 0800110064 (bure) au 0735 202 121(WhatsApp tu)

Imetolewa na 
Kitengo cha Mawasiliano