Wizara ya Maji

Dar es Salaam Water Supply And Sanitation Authority (DAWASA)

TIRA Logo
TAARIFA KWA UMMA - KUPUNGUA KWA UZALISHAJI MAJI KATIKA MTAMBO WA RUVU JUU
02 Mar, 2025 Pakua

TAARIFA KWA UMMA

KUPUNGUA KWA UZALISHAJI MAJI KATIKA MTAMBO WA RUVU JUU

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) inawataarifu Wananchi  na Wateja wanaohudumiwa na mtambo wa kuzalisha Maji Ruvu Juu uliopo Wilaya ya Kibaha kuwa, kumekuwa na upungufu wa huduma kutokana na matengenezo yanayoendelea katika miundombinu ya uzalishaji Maji katika Mtambo.

Kufuatia upungufu wa uzalishaji, maeneo yafuatayo yanapata Maji kwa msukumo mdogo:
 
Chalinze Mboga, Ruvu Darajani, Ruvu JKT, Vigwaza, Mlandizi, Mbwawa,Visiga, Maili 35, Misugusugu, Kongowe, Soga, Miembe Saba, Kwa Mfipa, Mwendapole, Tanita, Kwa Mathias, Kwa Mbonde, Picha ya Ndege, Lulanzi, Kibaha, Kiluvya, Kibamba, Mbezi, Magari Saba, Mbezi Inn, Mbezi, Kimara, Tabata, Segerea, Kinyerezi, Kisukuru, Bonyokwa, Msigani, Maramba Mawili, Kimara B, Kimara Korogwe, Bucha, Baruti, Ubungo, Magomeni, Ukonga, Uwanja wa Ndege, Kiwalani, Vingunguti, Gongo la Mboto, Pugu na Kisarawe

Tunaomba radhi kwa usumbufu utakaojitokeza.

Wasiliana nasi kupitia kituo cha huduma kwa wateja 0800110064 (bure) au 0735 202121 (WhatsApp Tu)

Imetolewa na 
Kitengo cha Mawasiliano