Wizara ya Maji

Dar es Salaam Water Supply And Sanitation Authority (DAWASA)

TIRA Logo
TAARIFA KWA UMMA - MATENGENEZO KINGA KATIKA MTAMBO WA MAJI RUVU CHINI
12 Mar, 2025 Pakua

TAARIFA KWA UMMA

MATENGENEZO KINGA KATIKA MTAMBO WA MAJI RUVU CHINI

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) inakusudia kufanya matengenezo kinga katika Mtambo wa Maji Ruvu Chini kwa lengo la kuimarisha huduma kipindi cha Mvua yatakayopelekea upungufu wa huduma ya maji kwa Saa 12 kwa Siku ya Alhamisi Machi 13, 2025.

Muda: Kuanzia Saa 12:00 Asubuhi hadi Saa 12:00 Jioni

Maeneo yatakayoathirika ni;

Bagamoyo, Mapinga, Mabwepande, Bunju, Tegeta, Kunduchi, Mbweni, Boko, Salasala, Goba, Mivumoni, Madale, Kawe, Lugalo, Makongo, Chuo Kikuu UDSM, Mwenge, Chuo Kikuu Ardhi, Kijitonyama, Mikocheni, Msasani, Oysterbay, Masaki, Mwananyamala, Kinondoni, Magomeni, Kigogo, Chang'ombe, Keko, Kurasini, Kigamboni, Airport, Kiwalani, Buguruni, Vingunguti, Ilala hadi Katikati ya Jiji.

Tunaomba radhi kwa usumbufu utakaojitokeza.

Wasiliana nasi kupitia kituo cha huduma kwa wateja 0800110064 (Bure) au 0735 202 121 (WhatsApp Tu)

Imetolewa na 

Kitengo cha Mawasiliano