Wizara ya Maji

Dar es Salaam Water Supply And Sanitation Authority (DAWASA)

TIRA Logo
TAARIFA KWA UMMA - ZOEZI LA USOMAJI MITA ZA MAJI KUANZA MACHI 10 - 15, 2025
10 Mar, 2025 Pakua

TAARIFA KWA UMMA 

ZOEZI LA USOMAJI MITA ZA MAJI KUANZA MACHI 10 - 15, 2025

Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) inawataarifu Wateja na Wananchi katika Mikoa ya Dar es Salaam na Pwani, kuwa zoezi la usomaji wa mita za maji linaanza Machi 10 hadi 15, 2025. 

Baada ya zoezi la usomaji mita kukamilika, Mteja atapokea ujumbe wa kuhakiki usomaji wa mita yake kabla ya bili kutumwa.

Kwa taarifa zaidi wasiliana nasi kituo cha huduma kwa wateja 0800110064 (Bure) na 0735-202121 (WhatsApp tu)

Imetolewa na 
Kitengo cha Mawasiliano