TANGAZO LA DHARURA - UPUNGUFU WA HUDUMA YA MAJI KWA WAKAZI WA MLANDIZI HADI KISARAWE
TANGAZO LA DHARURA
UPUNGUFU WA HUDUMA YA MAJI KWA WAKAZI WA MLANDIZI HADI KISARAWE
7.10.2024
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) inawatangazia Wateja na Wananchi wa maeneo ya Mlandizi hadi Kisarawe wanaohudumiwa na mtambo wa kuzalisha Maji Ruvu Juu kuwa, kutakuwa na upungufu wa huduma ya Maji kutokana na hitilafu katika Mtambo.
Maeneo yanayoathiri na upungufu wa huduma ni;
Chalinze, Mboga, Ruvu Darajani, Ruvu JKT, Vigwaza, Mlandizi, Mbwawa, Visiga, Maili 35, Misugusugu, Kongowe, Soga, Miembe Saba, Kwa Mfipa, Mwendapole, Tanita, Kwa Mathias, Kwa Mbonde, Picha ya Ndege, Lulanzi, Chanyikeni, Kibaha, Kiluvya, Kibamba, Mbezi, Magari Saba, Mbezi Inn, Mbezi, Kimara,Tabata, Segerea, Kinyerezi, Kisukuru, Bonyokwa, Msigani, Maramba Mawili, Kibangu, Kimara, Ubungo, Magomeni, Ukonga, Uwanja wa Ndege, Kiwalani, Vingunguti, Gongo la Mboto, Pugu na Kisarawe
Huduma inatarajiwa kuimarika mapema leo Mchana ,Oktoba 7,2024.
Tunaomba radhi kwa usumbufu utakaojitokeza.
Kituo cha huduma kwa wateja 0800110064 (bure) na 0735 202121 (WhatsApp Tu)
Imetolewa na
Kitengo cha Mawasiliano